Umasikini katika taifa letu umekuwa si jambo la kuwashangaza tena watu tunaowaamini,na ambao kwanamna moja ama njingine tuna aminini ndio injini ya kusaidia au kuchochea mabadiliko ya maendeleo katika jammii.
Mfanoo wa watuhao kama Wasomi, wataalam wa maswala mbali mbbali,wanasheria, waalimu wadini, na watu wenye weledi wowote kwenye maswala mbalimbali ya nayo muhusu mwananchi. Kwanamna moja ama nyingingene, hawaoni au hawaguswi na matatizo moja kwa moja ya nao wakabili vijana katika kujikwamua na ugumu wa maisha unao wakabili.
Kuthibitisha haya niyasemayo, ni jinsi watu wote tulivyo kaa kimya tunapo shindwa kuwa na mikakati endelevu ya kuwajengea vijana uwezo hasa wanaotoka vyuoni, au ambao wako mtaani.
Tumekosa mbinu mujarabu yakuhakikisha hii rasirimali watu tunaitengenezea utaratibu mzuri ili ijikite kwenye uzalisha, nakusaidia nchi kupata maaendeleo ya haraka.
Binafsi sitaki kujikita katika muendelezo wa kulaumu mambo yalivyo au kuu laumu mfumo unao tuongoza kwanama tunavyo weza kuwasaidia au kujisaidia sisi sote kama taifa.
Hapa chini nimejaribu kuja na angalau njia kadhaa ambazokwa namnamoja au njingine kama zita tumiwa au kufutwa na vijana zinawezakuwafanya ua kuwajengea vijana uwezo.,ili waweze kukabiliana nachangamoto za maisha zinazo wakabili.
KWANZA VIJANA WAJITAIDI KUTAFUTA TAARIFA SAHII NA ZA WAKATI.
Taarifa sahii ndizo msingi wakufanya mambo vizuri na kufikia mafanikio endelevu, ya mtu mmoja mmoja au taifa kwaujumla, swali lamsingi lakujiuli tarifa sahii tunazipata wapi?
Majibu ya swali hilo ni mepesi kabisa, taarifa sahii zinapatikana kwenye sekta husika, aushughulihussika, kwa mfano, unajiandakufungua kiwandakidogo cha usindikaji wa maziwa, nivizuri kupata maelekezo mazuri yana mna ya kuanzisha viwanda vidogo kwa watu kama SIDO wanao husika na viwanda vidogo vidogo. Taarifa ya SIDOitakuwa ni mwongozo mzuri kwamaendeleo ya kazi yako.
VJANA TUJIKITE KWENYE MAMBO YA MAANA.
Kwa namnamoja au njingine vijana tumepoteza muda mwingi kwenye mambo ambayo hayana tija kwetu wala kwa taifa, atupendi kudadisi mambo,tunaamini mambo yalivyo tubasi inatosha, tunapoteza rasilimali, muda, fedha na mabo kama hayo, mfano kijana ambaye hana kazi ya kueleweka anakuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijanazaidi ya mmoja, hali hii wakati mwingine inatulazimu kutumia muda mwingi, na tunapoteza pesa nyingi na tunapata faida hasi kwenye matokeo hayo.
TUTENGENEZE MTANDAO WENYE MANUFAA.
Mtandao ni njia moja wapo inayo tuwezesha kuendesha mambo yetu kwa manufaa yetu, na taifaletu.
Mtandao una tuwezesha kupata hata taarifasahii kwa ajili ya manufaa yetu. Niimaniyangu kwako kijana mwezangu kwamba kwa kupata taarifa sahii zitakuwa mwongozo sahihi kwa mambo yako. Mfano unahudhuria semina,au maonesho ya sabasaba ni vizuri kuchukua mawasiliano yawatumbali mbalimbali kutegemea na taarifa unazo hitaji kulingana nashughuli yako, au uliyo panga kuifanya, mara nyingi tumetengeneza au tuna endelea kutengeneza mitandao yakututoa pesa zaidi badala ya kutengeneza mitandao ya kuingiza pesa zaidi kwa maendeleo yetu.
TUJITAIDI KUPATA ELIMU NA TUPENDE KUSOMA TUKUZE FIKRA ZETU.
Shule ni mwalimu mzuri ili kufanikisha jambo kwa uhakika, tatizokubwa niliona lo kwa watanzania wote kuona elimu kama mzigo wa mawe, kwamba nikitu cha shida sana na kina uwekezaji mkubwa sana.
Hili lina wezakuwa ni jambo lakweli kutokana na mifumo yetuya kupata elimu na utoaji wake kwa jamii yetu. Elimu ilionekana, na bado inaoneka na kama anasa kuipata, na upatikanaji wake ni mgumu sana, inaonekana ni kwa watu wenye hela tu wanaowezakuipata, na ni kwatabusana.
Pamoja na yote hayo iyo isitumike kama sababu ya kimantiki kufifisha ari na hitaji la mtu mmoja mmoja kupata elimu. Lazma mamlaka husika na sisi wananchi mmoja mmoja tuwe na hamu ya kupata elimu na tuitafute kokote kwa udi na uvumba, kwani elimu bora ndio mstakbali wabaadae yetu.
Kwa leoni hayo machache ndugu kijana mwezangu, tujitaidi kubadilika kifikra,
Sisi sote ni ndugu.
Na Godfrey Nangeda.